Mazingira FM

Bunda: Mvuvi atumbukia ziwa Victoria, siku ya tatu hajapatikana

9 February 2025, 10:11 pm

Baadhi ya wananchi na wanafamilia wakiwa kando ya ziwa Victoria wakishuhudia zoezi la utafutaji wa aliyezama maji (Picha na Yohana)

By Edward Lucas

Mtu mmoja Aliyefahamika kwa jina la Kusekwa Fanuel Rufundya (31) mkazi wa mtaa wa Ihale kata ya Guta anahofiwa kufariki dunia kwa kuzama ndani ya maji wakati akiwa katika shughuli za uvuvi ziwa victoria kata ya Guta halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara.

Mwenyekiti wa mtaa wa Guta Mjini, Steven Malweta Mabusi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Ijumaa tarehe 7 Feb 2025 majira ya saa 02:00 asubuhi wakati mtu huyo akiwa kwenye mashua (mtumbwi) na wenzake wawili wakiendelea na shughuli za uvuvi ndipo ghafla alitoweka na juhudi za wenzake kuanza kumtafuta zilizanza kwa haraka bila ya mafanikio yoyote

Steven Malweta Mabusi, mwenyekiti wa mtaa

Misoji Rufundya ni Mama mkubwa wa Kusekwa Rufundya ambaye yuko katika eneo la tukio ameeleza kwa namna alivyopokea taarifa ya kijana wao kuzama majiniI

Misoji Rufundya