Mazingira FM

Diwani Mramba awezesha 12 kwenda shule

17 January 2026, 5:11 pm

Hii ikiwa inafikia  jumla ya wanafunzi 160 wanaosaidiwa na diwani huyo .

Na Adelinus Banenwa

Wakati serikali ikiwahimiza wazazi na walezi kuhakikisha Watoto wote waliofaulu kufika shuleni hatakama mahitaji wadau mbalimbali wameendelea kusaidia vifaa vya shule kwa baadhi ya Watoto wanaoishi katika mazingira magumu

Mramba Simba Nyamkinda diwani wa kata ya Ketare halmashauri ya wilaya ya Bunda hii leo Jan 17, 2026, ametoa vifaa kwa wanafunzi 12 wa shule ya sekondari ya Esperanto wanaoishi katika mazingira magumu na hii ikiwa inafikia  jumla ya wanafunzi 160 wanaosaidiwa na diwani huyo .

Sauti ya Mramba Simba Nyamkinda

Aidha mhe mramba ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwahimiza  Watoto wao kuzingatia masomo , na wanafunzi wenyewe kuweka juhudi katika masomo

Sauti ya Mramba Simba Nyamkinda

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi waliopata msaada  huo wamemshukuru mhe mramba kwa kuwawezesha kupata vifaa vya shule na kuahidi kusoma kwa bidii ili kutimiza ndoto zao.

Sauti ya wanafunzi