Mazingira FM

Makaburi hewa changamoto kwenye mradi wa tanesco Bunda

6 January 2026, 9:09 pm

Zoezi uamishaji wa makaburi likiendelea

Msaki amesema katika zoezi hilo wanakumbana na changamoto kadhaa ikiwemo watu kutaja makaburi ambapo ukichimba unakuta hamna kitu hivyo kuwepo kwa makaburi hewa.

Na Adelinus Banenwa

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda mkoani Mara imeanza zoezi la uhamishaji wa makaburi ili kupisha ujenzi wa mradi wa njia ya umeme wa Bunda – Ukerewe.

Magreth Nyambwa ambaye Afisa afya halmashauri ya wilaya ya Bunda amesema katika zoezi hilo wanatarajia kuhamisha jumla ya makaburi 61 ambayo yapo kwenye vijiji 11 kwa halmashauri ya wilaya ya Bunda ambavyo ni , Bulendabufye, Bulamba, Chitengule, Igundu, Kisorya, Mahyoro, Makwa, Masaunga, Mwibara, Namibu na Nampangala.

Magreth amesema zoezi hilo limeanza tangu tarehe 15 Dec 2025 kwa kupita nakutambua makaburi hayo kisha leo Jan 6 zoezi la uamishaji linaendelea ambapo kwa siku ya kwanza tayari vijiji vinne vimefikiwa kati ya vijiji 11.

Sauti ya Magreth Nyambwa Afisa afya halmashauri ya wilaya ya Bunda
Zoezi la uhamishaji wa makaburi likiendelea

Nasri Msaki mpima Ardhi kutoka shirika la umeme Tanzania TANESCO amesema umeme huo utakuwa wa Msongo wa Kilovoti 132 kutoka Gridi ya taifa na njia hiyo kutoka bunda hadi ukerewe una urefu wa Kilometa 98 na upana wa njia hiyo utakuwa ni mita 27 ambapo wananchi wote waliopitiwa na mradi huo 1298 na kati ya hao wananchi 1179 tayari wamelipwa fidia zao na wachache waliobaki ni kwasababu mbalimbali.

Sauti ya Nasri Msaki mpima Ardhi kutoka Shirika la Umeme Tanzania TANESCO

Msaki amesema katika zoezi hilo wanakumbana na changamoto kadhaa ikiwemo watu kutaja makaburi ambapo ukichimba unakuta hamna kitu hivyo kuwepo kwa makaburi hewa pia changamoto ya baadhi ya ndugu kudai hawana sehemu ya kwenda kuwahifadhi ndugu zao kutokana na maeneo yao yote kuchukuliwa katika mradi huo.

Sauti ya Nasri Msaki mpima Ardhi kutoka shirika la umeme Tanzania TANESCO
Baadhi ya makaburi yaliyohamishwa

Kwa upande wao baadhi ya ndugu waliokuwa wanahamisha miili ya ndugu zao wamesema wameridhishwa na zoezi lilivyoendeshwa kwa kuwa wameshirikishwa kila hatua.

Sauti ya baadhi ya ndugu waliokuwa wanahamisha miili ya ndugu zao