Mazingira FM

Wakulima kutumia kilimo mseto kukabili mabadiliko ya tabianchi

11 December 2025, 5:22 pm

Afisa kilimo Elton Dickson Mtani akiwa studio za radio Mazingira FM,picha na Catherine Msafiri.

Afisa kilimo Elton Dickson Mtani kilimo mseto ni miongoni mwa mbinu bora zinazoweza kuwasaidia wakulima kukabiliana na changamoto zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.

Na Catherine Msafiri,

Katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi wakulima wameshauriwa kutumia kilimo mseto kama njia moja wapo.

Afisa kilimo Elton Dickson Mtani amesema kuwa kilimo mseto ni miongoni mwa mbinu bora na za kisasa zinazoweza kuwasaidia wakulima kukabiliana na changamoto zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.

Akizungumza katika mahojiano kwenye kipindi cha uhifadhi  wa mazingira kupitia radio Mazigira FM Mtani alisema kilimo mseto ambacho kinahusisha kulima mazao zaidi ya aina moja katika shamba moja kama mazao ya chakula ,upandaji wa miti na ufugaji mdogo .

Sauti ya Afisa kilimo Elton Dickson Mtani

 Mtani alifafanua kuwa kuna aina za miti ambayo inashauriwa kupandwa kwenye shamba ili kusaidia kuongeza rutuba Pia aliwataka wakulima kuzingatia kilimo hifadhi.

Sauti ya Afisa kilimo Elton Dickson Mtani

Mwisho, aliwahimiza wakulima kupata ushauri kutoka kwa maafisa kilimo wa maeneo yao ili kupata mwongozo sahihi wa namna ya kupanga mazao na kutekeleza kilimo mseto kwa ufanisi.