Mazingira FM

Wananchi waaswa kushiriki mbio za utalii, mazingira

24 November 2025, 6:44 pm

Halid Omary meneja wa yas Mara ya kusini

Wanaotaka kushiriki Serengeti Safari Marathon walipie mix by yas shilingi 45 kwa mbio za kilometa 5,21 na 42.

Na Catherine Msafiri,

Yas wamesema wataendelea kudhamini shughuli mbalimbali za kijamii ikiwa ni Sehemu ya kurudisha shukurani kwa wateja wao.

Hayo yamesemwa na Halid Omary meneja wa yas mkoa wa Mara kwenye uzinduzi wa Serengeti Safari Marathon msimu wa nane ambao umefanyika katika makumbusho ya baba wa Taifa Mwitongo Butiama mkoani Mara lengo likiwa ni kufanya mbio za kiutalii ndani ya hifadhi ya taifa Serengeti.

Omary amewaasa wananchi kutokeza kushiriki mbio hizo kwani ni fursa ya kufanya mazoezi,utalii na utunzaji wa mazingira kwani kila mshiriki atapewa mbegu za asili 20 za miti kwaajiri ya kupanda ili kutunza mazingira.

Baadhi ya wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Serengeti Safari Marathon,picha na Catherine Msafiri.

Aidha amebainisha kuwa mtu anaweza kujisajili kwa kulipia kupitia mix by yas shilingi 45 kwa mbio za kilometa 5,21 na 42

Sauti ya Halid Omary meneja wa yas Mara ya kusini
Mkuu wa wilaya ya Butiama Bi.Tecla Mkuchika kwenye uzinduzi wa Serengeti Safari Marathon,picha na Catherine Msafiri

Mkuu wa wilaya ya Butiama Bi.Tecla Mkuchika amezindua rasmi mbio hizo akiwaasa wananchi kulinda amani , ameeleza kuwa mbio za serengeti safari marathon zinafanyika kama hamasa ya utalii kutokana na mbio hizo kufanyika ndani ya hifadhi huku wakihamasisha utunzaji wa mazingira.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Butiama Bi.Tecla Mkuchika

Serengeti safari marathon msimu wa nane umezinduliwa leo huku kilele ni tarehe 29 November 2025 ikiwa na kaulimbiu isemayo “Tourism Connect“ ikiwa na maana ya utalii unganishi.