Mazingira FM

Lishe duni kwa mjamzito kichocheo cha kuzaliwa mtoto njiti

18 November 2025, 12:54 pm

Rehema Kapile  afisa lishe na mratibu wa elimu ya afya kwa umma Bi.Magreth Arbogast wakiwa studio za radio Mazingira FM,picha na Catherine Msafiri.

Rehema Kapile  afisa lishe makundi yote sita ya vyakula ni rahisi kupata na hata kwa jamii zenye uchumi wa chini hivyo wajawazito watumie ili kuepukana na athari zinazoweza kutokea akiwa na lishe duni.

Na Catherine Msafiri,

Ukosefu wa lishe bora kwa mama mjamzito yatajwa kunaweza kupelekea mama kupoteza ujauzito au kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo ama mtoto njiti

Hayo yameelezwa na Rehema Kapile  afisa lishe kutoka Halmshauri ya wilaya ya Bunda wakati akizungumza kwenye kipindi cha kapu letu kutoa elimu kuhusu umuhimu wa lishe kwa mama mjamzito ambapo ameeleza kuwa lishe ni muhimu kwa mama mjamzito kwa faida yake na mtoto

Rehema Kapile  afisa lishe Halmashauri ya wilaya ya Bunda akiwa studio za Mazingira FM,picha Catherine Msafiri

Rehema amebainisha kuwa yapo makundi sita ambayo mama mjamzito anashauriwa kutumia makundi ya vyakula vyenye protini,vyakula vya wanga (carbohydrates),mboga za majani,matunda ,maziwa na bidhaa zake ,vyakula vyenye madini na vitamini ni muhimu kwa mtoto aliyepo tumboni

Sauti ya Rehema Kapile  afisa lishe Halmashauri ya wilaya ya Bunda

Aidha Rehema ameeleza kuwa makundi yote hayo ya vyakula ni rahisi kupata na hata kwa jamii zenye uchumi wa chini hivyo wajawazito watumie ili kuepukana na athari zinazoweza kutokea kama za kupoteza mtoto ,kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo au mama kupoteza maisha

Sauti ya Rehema Kapile  afisa lishe Halmashauri ya wilaya ya Bunda

Aidha kwa upande wake mratibu wa elimu ya afya kwa umma kutoka Halmashauri ya wilaya ya Bunda Bi.Magreth Arbogast amesema wanatoa elimu ya lishe kwa jamii ili kuwawezesha wajawazito kuwa na lishe bora wakati wa ujauzito mpaka anapojifungua.

Sauti ya mratibu wa elimu ya afya kwa umma Bi.Magreth Arbogast

Hata hivyo wameeleza vitu ambavyo mama mjamzito hapaswi kutumia wakati wa ujauzito.

Sauti ya mratibu wa elimu ya afya kwa umma Bi.Magreth Arbogast na Rehema Kapile  afisa lishe