Mazingira FM

Kapigeni kura hakuna tishio la usalama; DC Aswege

24 October 2025, 1:38 pm

uu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswenge Enock Kaminyoge

Jumla ya wapigakura wenye sifa kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ni takribani watu 253.891

Na Adelinu Banenwa

Mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswenge Enock Kaminyoge amewahakikishia wananchi wilayani Bunda ambao wanasifa za kupiga kura tarehe 29 oct kwenda kutimiza haki yao ya kikatiba kwa kuwa hali ya usalama imeimalishwa.

baadhi ya viongozi wa dini walioudhuria kikao cha mkuu wa wilaya ya Bunda

Akizungumza na viongozi wa dini leo tarehe 23 oct 2025 DC Aswege amesema viongozi wa dini wanayo nafasi ya kwenda kuzungumza na waumini wao juu ya kushiriki uchaguzi mkuu kutokana na umuhimu wake ambao kupitia uchaguzi huo watapatikana viongozi watakaowaletea maendeleo

Sauti ya Mhe Aswenge Enock Kaminyoge

Ameongeza kuwa katika majimbo matatu ya wilaya ya Bunda jumla ya wapigakura wenye sifa kwa mujibu wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ni takribani watu 253.891 ambapo kati yao jimbo la Bunda Mjini ni 110,674 jimbo la Bunda ELFU 58,907 na jimbo la Mwibara ni 84,310

Sauti ya Mhe Aswenge Enock Kaminyoge
Kiongozi wa kidini katika kikao cha mkuu wa wilaya

Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa dini wameishauri serikali kushughulikia changamoto za wananchi ili kupunguza hasira na manung’uniko miongoni kwa changamoto zingine hasa katika huduma za kijamii ikiwemo afya elimu n.k

Sauti za baadhi ya viongozi wa dini