Mazingira FM

Hali ya usalama Mara ni shwari, Kamanda Lutumo

16 October 2025, 3:22 pm

Kamanda wa polisi mkoa wa Mara Pius Lutumo

Jeshi la polisi limesema limeshajiandaa kikamilifu  kusimamia usalama wakati wa uchaguzi kama wanavyofa katika kipindi hiki cha kampeini.

Na Adelinus Banenwa

Jeshi la polisi mkoa wa Mara limewahakikishia wananchi wote mkoani Mara kuwa hali ya usalama ni nzuri na jeshi kinaendelea kushirikiana na wananchi kuimarisha usalama huo.

Hayo yamesemwa na kamanda wa polisi mkoa wa Mara Pius Lutumo alipozunzumza na Radio Mazingira FM kupitia kipindi cha Asubuhi leo ambapo amesema jeshi hilo kupitia program ya polisi jamii angalau kila kata kuna polisi kata mwenye cheo  angalau cha mkaguzi msaidizi wa polisi.

Kamanda Lutumo amesema lengo likiwa ni kutoa elimu na kushirikiana na wananchi kudhibiti matukio ya kiharifu kwenye jamii.

Sauti ya kamanda wa polisi mkoa wa Mara Pius Lutumo

Kuelekea uchaguzi mkuu Oct 29 kamanda Lutumo amewahakikishia wananchi hali ya usalama kuwa shwali huku akisisitiza kuwa  wao kama jeshi la polisi umeshajiandaa kikamilifu  kusimamia usalama kama wanavyofa katika kipindi hiki cha kampeini

Sauti ya kamanda wa polisi mkoa wa Mara Pius Lutumo