Mazingira FM

Wananchi waaswa kuepuka kufuata mikumbo

6 October 2025, 6:38 pm

Wakili Msomi Kabengwe Matiasi Kabengwe, ambaye pia ni Mrakibu wa Polisi Mkoa wa Mara

Wananchi wanapaswa kuwa na utamaduni wa kutafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa sheria, wakiwemo mawakili.

Na Adelinus Banenwa.

Wananchi wameaswa kuacha tabia ya kufuata mikumbo katika kufanya maamuzi, kwani baadhi ya mambo yanayofanywa kwa mazoea au kwa ushawishi wa watu wengine yanaweza kuwasababishia matatizo ya kisheria bila wao kutarajia.

Wito huo umetolewa na Wakili Msomi Kabengwe Matiasi Kabengwe, ambaye pia ni Mrakibu wa Polisi Mkoa wa Mara, wakati akizungumza katika kipindi cha Ufahamu wa Sheria kinachorushwa na Radio Mazingira FM.

Sauti ya Wakili Msomi Kabengwe Matiasi Kabengwe,

Wakili Kabengwe amesema wananchi wanapaswa kuwa na utamaduni wa kutafuta ushauri kutoka kwa wataalamu wa sheria, wakiwemo mawakili, ili kupata ufafanuzi wa kisheria pale wanapokumbana na changamoto mbalimbali katika jamii.

Sauti ya Wakili Msomi Kabengwe Matiasi Kabengwe,
Wakili Msomi Kabengwe Matiasi Kabengwe, ambaye pia ni Mrakibu wa Polisi Mkoa wa Mara

Aidha, amesema kuwa kupitia Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kumekuwa na utaratibu wa kutoa msaada wa kisheria bure kwa watu wasiokuwa na uwezo wa kugharamia huduma za mawakili, hususan kwenye kesi kubwa kama zile za mauaji.

Sauti ya Wakili Msomi Kabengwe Matiasi Kabengwe,

Wakili huyo amehitimisha kwa kusisitiza kuwa elimu ya kisheria ni muhimu kwa kila mwananchi, kwani inasaidia kujenga jamii inayofuata sheria, haki na utulivu.