Mazingira FM

Uelewa wa jamii kuhusu uzazi wa mpango

29 September 2025, 1:27 pm

Mariam Nyangi, muuguzi wa afya kituo cha AICT Bunda

Sikiliza makala haya maalumu kuhusu uelewa wa jamii kuhusu uzazi wa mpango hatua ya kujenga jamii na uchumi.

Na Dinnah Shambe

Katika jamii nyingi, suala la uzazi wa mpango limeendelea kuwa jambo lenye mjadala mkubwa, hasa kutokana na mitazamo tofauti ya kitamaduni, kijamii, na kidini. Watu wengi bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu maana, umuhimu na faida za uzazi wa mpango. Hali hii huathiri kwa kiasi kikubwa ustawi wa familia na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Katika makala haya ya dakika 15 tumezungumza na jamii kujua mtizamo wao kuhusu  Uzazi wa mpango ambao  ni haki ya msingi ya kila mtu inayomuwezesha mwanamke au mwanaume kupanga idadi ya watoto wanaotaka, muda wa kupata mtoto mwingine, na aina ya maisha wanayoyapanga kama familia

  Sikiliza makala hii maalimu kuhusu uelewa wa jamii kuhusu uzazi wa mpango hatua ya kujenga jamii na uchumi.