Mazingira FM

Kaya zaidi 125 kunufaika na usambazaji maji Miembeni

18 September 2025, 5:49 pm

Baadhi ya mabomba yatakayotumika kwenye huduma ya usambazaji maji mtaa wa Miembeni Ukanda wa Gaza yakishushwa eneo la mradi.

Wakazi wa mtaa huo wa Miembeni wameishukuru Serikali na mamlaka ya maji Bunda kwa kuwakumbuka kuwafikishia huduma ya maji safi

Na Adelinus Banenwa

Zaidi ya kaya 125 kata ya  Bunda stoo mtaa wa miembeni maarufu  Ukanda wa Gaza kunufaika na mradi wa usambazji maji kutoka mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Bunda BUWSSA.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa mamlaka hiyo Bi Esther Gilyoma wakati akikabidhi mabomba kwa wakazi hao ambayo yametolewa na serikali kupitia mamlaka hiyo huku akiongeza kuwa kwa sasa mamlaka inaendelea na miradi  mitano ukiwemo mradi wa Maji taka,Mradi wa  usambazaji maji wa Kisangwa, Mradi wa usambazaji maji Wariku, mradi wa maji Nyamuswa na mradi wa kupambana na upotevu wa maji wa bomba kuu kwenda mlima kaswaka.

Baadhi ya mabomba yatakayotumika kwenye huduma ya usambazaji maji mtaa wa miembeni ukanda wa gaza kiwa saiti

Aidha Bi Gilyoma amesema  mradi huo wa usambazaji maji  eneo la Ukanda wa Gaza mtaa wa Miembeni utakuwa na urefu wa zaidi ya kilometa 2 na kutakuwa na vituo viwili vya kuchotea maji yaani DPs.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa BUWSSA Bi Esther Gilyoma

Kwa upande wao wakazi wa mtaa huo wa Miembeni wameishukuru Serikali na mamlaka ya maji Bunda kwa kuwakumbuka kuwafikishia huduma ya maji safi kwa kuwa tangu uhuru eneo hilo halijawahi kupata huduma ya maji safi

Mkurugenzi mtendaji wa BUWSSA Bi Esther Gilyoma katikati akiwa na watumishi wa mamlaka ya maji bunda pamoja na wakazi wa mtaa wa Miembeni

Wakazi hao wamesema wako tayari kushirikiana na BUWSSA hata kuchimba mitaro ili huduma hiyo iweze kuwafikia kwa haraka.

Sauti ya baadhi ya wakazi wa miembeni