Mazingira FM

Mwalimu: Nikiwa Rais nitafufua kilimo, kujenga viwanda

11 September 2025, 8:57 pm

Salumu Mwalimu Mgombea urais kupitia chama cha ukombozi wa umma CHAUMA

Utajiri uliopo nchini Tanzania kwa wingi la rasilimali zilizopo yakiwemo madini, mito maziwa na bahari, ardhi yenye rutuba miongoni mwa rasilimali zingine

Na Adelinus Banenwa

Mgombea urais kupitia chama cha ukombozi wa umma CHAUMA Salumu Mwalimu amesema endapo atachaguliwa katika uchaguzi wa mwezi October kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania atahakikisha anajenga viwanda mkoani Mara na kuimarisha sekta ya kilimo ili kukuza ustawi wa wananchi na kuongeza ajira.

Salumu Mwalimu Mgombea urais kupitia chama cha ukombozi wa umma CHAUMA akizungumza na baadhi ya wakazi wa Bunda baada ya mkutano wa kampeini

Mwalimu ameyasema hayo leo katika mkutano wake wa kampeni wilayani Bunda uliofanyika stendi ya zamani Mjini Bunda ikiwa ni mwendelezo wa kunadi sera za chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu.

Sauti ya mgombea urais kupitia chama cha ukombozi wa umma CHAUMA Salumu Mwalimu

Mbali na ahadi hizo Mwalimu amebainisha suala la utajiri uliopo nchini Tanzania kwa wingi la rasilimali zilizopo yakiwemo madini, mito maziwa na bahari, ardhi yenye rutuba miongoni mwa rasilimali zingine ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuwakwamua wananchi kiuchumi na kuondoa umasikini miongoni mwa watanzania.

Baadhi ya wakazi wa Bunda waliojitokeza kumsikiliza mgombea urais kupitia chama cha CHAUMA
Sauti ya mgombea urais kupitia chama cha ukombozi wa umma CHAUMA Salumu Mwalimu