Mazingira FM

Wagombea wahamasisha ‘amani, utulivu’ kuelekea uchaguzi 2025

19 August 2025, 8:39 pm

Msimamizi msaidizi wa uchaguzi kata ya Nyasura akimkabidhi fomu ya kugombea udiwani kupitia chama cha mapinduzi CCM ndugu Magigi Samwel Kiboko

Makada wa CCM wapishana ofisi za wasimamizi wasaidizi wa tume kuchukua fomu za kuwania udiwani

Na Adelinu Banenwa

Mgombea wa udiwani kata ya nyasura kupitia chama cha mapinduzi CCM ndugu Magigi Samwel Kiboko amewaomba wanachama wa chama hicho kuwa watulivu na kuepuka vurugu katika kipindi chote kuelekea uchaguzi mkuu 2025.

Magigi ameyasema hayo leo tarehe 19 Aug 2025 baada ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo kwa msimamizi msaidizi watume huru ya taifa ya uchaguzi kwa kata ya Nyasura.

Sauti ya Magigi Samwel Kiboko
Msimamizi msaidizi wa uchaguzi kata ya Kabarimu akimkabidhi fomu ya kugombea udiwani kupitia chama cha mapinduzi CCM ndugu Kulwa Ramadhan Ngata

Wakati huo huo mgombea wa chama hicho cha mapinduzi kwa kata ya Kabarimu ndugu Ramadhan Kulwa Ngata amewataka wanachama wote wa CCM kuwa na umoja na mshikamano kuelekea uchaguzi mkuu huku akisisitiza kuwa umoja wao ndiyo ushindi.

Ngata pia ameyasema hayo mbele ya ofisi ya msimamizi msaidizi wa tume huru ya taifa ya uchaguzi kwa kata ya kabarimu baada ya kuchukua fomu ya kuwania udiwani wa kata hiyo kupitia CCM,

Sauti ya Kulwa Ramadhan Ngata