Mazingira FM

Miaka miwili baada ya mume kujinyonga, mke naye ajinyonga

22 July 2025, 8:18 pm

Tukio la mama huyo kujinyonga limeacha maswali mengi kutokana na mume wake miaka miwili iliyopita alifariki kwa kujinyonga pia

Na Adelinus Banenwa

Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Pili Chacha (40) amefariki dunia kwa kujinyonga kwenye mti ulipo pembezoni mwa nyumba yake mtaa wa Migungani Bunda mjini

Mti uliyotumiwa na wanandoa wawili kujinyongea kwa nyakati mbili tofauti

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema majira ya saa tano asubuhi walisikia kilio kutokea kwenye nyumba ya mama huyo na walipofika walikuta ni binti yake analia huku na kionesha kwenye kichaka pembeni mwa nyumba ambapo mama huyo alikuwa ameninginia.

Sauti za mashuda

Kwa upande wake Raitony Aloyce ambaye ni shemeji wa marehemu ameiambia mazingira fm kuwa tukio la shemeji yake kujinyonga limewauzunisha ambapo amesema marehemu ameacha watoto sita huku akisema hadi sasa familia haijui nini chanzo cha mama huyo kuchukua maamuzi hayo.

SaRaitony Aloyce

Mwenyekiti wa mtaa wa Migungani kata ya Bunda stoo halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara Jafeth Ryoba Marco amesema ni kweli tukio hiyo limetokea leo na baada ya kupewa taarifa na mtendaji aliwajulisha polisi waliofika eneo la tukio na kufanya vipimo kisha kukabidhi mwili kwa ndugu kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi .

Baadhi ya wananzengo wakiwa msibani kwa Pili Chacha

Jafeth amesema tukio la mama huyo kujinyonga limeacha maswali mengi kutokana na mume wake miaka miwili iliyopita alifariki kwa kujinyonga pia hivyo kama wanamtaa na viongozi wamebaki na maswali

Sauti ya Jafeth Ryoba Marco