Mazingira FM

Msimu wa pamba wafunguliwa Bunda AMCOS, wapewa onyo kali

29 May 2025, 7:54 pm

Mkaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda ndugu Hemedi Kabea, akifafanua baadhi ya miongozo kwa wadau wa zao la pamba kuelekea msimu wa ununuzi wa zao la pamba mwaka 2025 na 2026

Kwa mujibu wa muongozo uliopo wakulima wote wa zao la pamba wamesamehewa madeni ya mkopo wa pembejeo.

Na Adelinus Banenwa

Katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela amewaagiza AMCOS kujiepusha na udanganyifu wa kilo za pamba kwa lengo la kukwepa ushuru unaotakiwa kulipwa .

Mtelela ameyasema hayo katika kikao cha wadau wa zao la pamba wilayani Bunda kilichoketi kwa lengo la kuwapatia AMCOS mikataba pamoja na maelekezo kuelekea ufunguzi wa ununuzi wa zao la pamba wilayani Bunda

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela

Kwa upande wake mkaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda ndugu Hemedi Kabea amesema kwa mujibu wa muongozo uliopo wakulima wote wa zao la pamba wamesamehewa madeni ya mkopo wa pembejeo,  hivyo ni marufuku kwa kiongozi wa AMCOS yeyote  kumkata mkulima fedha ya mkopo wa pembejeo.

baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha pamba wakiwemo viongozi wa AMCOS Bunda
Sauti ya mkaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda ndugu Hemedi

Naye meneja wa bodi ya pamba mkoa wa Mara Baraka Kiboye amesema kampuni itakayokuwa inapandisha bei ya pamba hiyo ndiyo itakayokuwa inanunuliwa pamba kwenye AMCOS .

Pia ameongeza kuwa inapotokea kuna mabadiliko ya bei viongozi wa AMCOS wanatakiwa kusaini ili kuepuka mkono wa sheria kwa kujaribu kwaibia wakulima.

Sauti ya meneja wa bodi ya pamba mkoa wa Mara Baraka Kiboye