Mazingira FM

Vijana wahimizwa kugombea uchaguzi mkuu 2025

24 May 2025, 8:41 pm

Katibu UVCCM wilaya ya Bunda Pendo Machilu

Ni jukumu la vijana hao kuhakikisha wanwalinda viongozi pia wanajitokeza kugombea nafasi za uongozi pindi mchakato wa chama utakapoanza

Na Adelinus Banenwa

Katibu wa jumuiya ya umoja wa vijana chama cha mapinduzi wilaya ya Bunda Pendo Machilu amewataka vijana kuacha woga na kujitokeza kugombea nafasi za uongozi kwa udiwani na ubunge katika uchaguzi mkuu wa 2025.

Pendo ameyasema hayo leo May 24 2025 wakati akizungumza kwenye baraza la umoja wa vijana CCM kata ya nyamakokoto ambapo amesema ni jukumu la vijana hao kuhakikisha wanwalinda viongozi pia wanajitokeza kugombea nafasi za uongozi pindi mchakato wa chama utakapoanza.

Sauti ya KatibuUVCCM wilaya ya Bunda Pendo Machilu

Kwa upande wake mwenyekiti wa umoja huo kwa kata ya Nyamakokoto ndugu Anthony Dickson amesema ujumbe alioutoa katibu wa jumuiya hiyo wilaya ya Bunda umekuwa chachu kwa vijana waliokuwa na mashaka juu ya kugombea nafasi za uongozi

Aidha ndugu Anthony Dickson amewahimiza vijana wote kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili wawachague viongozi watakaowaletea maendeleo katika maeneo yao.

Sauti ya mwenyekiti wa UVCCMkata Nyamakokoto ndugu Anthony Dickson