Mazingira FM

Habibu: Usikate bima baada ya kupata matatizo

19 April 2025, 8:28 pm

Sheria ya bima inayatambua makundi matatu  ambayo ni taasisi inayotoa bima, taasisi, kampuni au mtu anayekata bima na kundi la tatu ni wanaopata majanaga ambao hawafungamani na makundi mawili ya awali

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa jamii kuondoa dhana ya kukata bima mara baada ya kupata majanga badala yake wakate bima mapema ili kuweka mazingira mazuri ya ulinzi wa vyombo  vyao vya moto pamoja na mali.

Hayo yamesemwa na Abdulhakimu Habibu afisa kutoka shirika la bima la taifa NIC mkoani Mara  tawila Musoma wakati akizungumza kupitia kipindi cha ufahamu wa sheria radio mazingira fm

Sauti ya Habibu

Aidha habibu amesema katika sheria ya bima inayatambua makundi matatu  ambayo ni taasisi inayotoa bima, taasisi, kampuni au mtu anayekata bima na kundi la tatu ni wanaopata majanaga ambao hawafungamani na makundi mawili ya awali

Sauti ya Habibu