Mazingira FM

Bunda kuadhimisha miaka minne ya Rais Samia Machi 17

15 March 2025, 5:46 pm

Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Miongoni mwa maeneo yatakayoangaziwa ni pamoja na sekta mbalimbali za serikali ikiwemo Maji, Umeme, Afya, Barabara pamoja na Elimu.

Na Adelinus Banenwa

Serikali wilayani Bunda imewaomba wananchi wote kuudhuria maadhimisho ya miaka minne ya serikali ya awamu ya sita chini ya rais Samia Suluhu Hassan yanatarajiwa kufanyika Tarehe 17 March 2025.

Akizungumza na radio mazingira fm ofisini kwake katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela amesema wananchi wote wanaalikwa siku hiyo ya jumatatu ambapo watapata nafasi ya kusikiliza kile serikali ya awamu ya sita imefanya ambapo mgeni rasmi atakuwa ni mkuu wa wilaya ya Bunda Mhe Aswege Enock Kamnyoge.

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Aidha Mtelela amesema ratiba ya maadhimisho hayo inatarajiwa kuanza na zoezi la upandaji miti katika eneo la Kunzugu kisha kwenye viwanja vya ukumbi wa Maika na miongoni mwa maeneo yatakayoangaziwa ni pamoja na sekta mbalimbali za serikali ikiwemo Maji, Umeme, Afya, Barabara pamoja na Elimu.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka minne ya rais Samia wilaya ya Bunda imepokea kiasi cha fedha za miradi zaidi ya Bilion 247 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Ikumbukwe Rais Samia Suluhu Hassan aliapishwa kuwa rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania mnamo March 19, 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake Hayati Dr John Pombe Magufuli Rais awamu ya tano.