Mazingira FM

Mbunge Maboto: Wazazi timizeni jukumu la chakula shuleni kuongeza ufaulu

25 February 2025, 9:00 am

Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto akikabidhi chakula katika baadhi ya shule kweye kampeni ya uchangiaji chakula shuleni

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Robert Chacha Maboto amewataka wazazi kujitolea katika kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni ili kuongeza hali ya taaluma.

Na Adelinus Banenwa

Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto amewataka wazazi kujitoa katika kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni ili kuongeza hali ya taaluma kwa shule za halmashauri ya mji wa Bunda.

Mhe Maboto amesema hayo tarehe 24 Feb 2025 katika ziara yake alipozitembelea jumla ya shule saba za sekondari za halmashauri ya mji wa Bunda kuhamasisha zoezi la uchangiaji wa chakula mashuleni.

Wanafunzi wakifurahia baada ya kupata chakula kutoka kwa Mhe mbunge Maboto

Mhe mbunge amesema maisha ya wakati huu ni tofauti na maisha ya zamani kutokana na mabadiliko mbalimbali ambapo zamani wazazi walitegemea mifugo na mashamba lakini kwa sasa kitu pekee ambacho mzazi anaweza kumrithisha mtoto wake kikamsaidia ni elimu tu.

Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto, akizungumza na baadhi ya wanafunzi.

Mhe Mbunge ametembelea shule za sekondari za Dkt Nchimbi, Manyamanyama, Kabasa, Wariku, Guta, Nyamakokoto na shule ya Sekondari ya Bunda mjini ambapo kila shule ametoa gunia 4 za mahindi, maharage pamoja na sukari kilo 25.

Sauti ya Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto
Moja ya wanafunzi akitoa shukrani kwa Mhe mbunge Robert Maboto kwa hamasa ya chakula shuleni

Kwa upande wao wanafunzi wameshukuru jitihada za Mhe mbunge kuwakumbuka kuwaletea chakula huku wakiahidi kusoma kwa bidii na kuwa chachu ya kuwahamasisha wazazi wao kupeleka chakula mashuleni.

Sauti za wanafunzi wakishukuru mbunge kwa kuwapatia chakula kama hamasa ya wazazi ili kuongeza ufaulu
Baadhi ya viongozi kata ya Nyasura

Baadhi ya viongozi wa maeneo husika wakizungumza katika ziara hiyo wameainisha juhudi wanazozifanya kuhakikisha wazazi wanaleta chakula shuleni ambapo hamasa hizo inaelezwa zinafanyika kupitia kwa viongozi wa kata pamoja na kamati za shule.

Baadhi ya sauti za madiwani
Baadhi ya sauti za wakuu wa shule
Afisa lishe halmashauri ya mji wa Bunda Lucy Mwalwayo

Afisa lishe halmashauri ya mji wa Bunda Lucy Mwalwayo amesema kushindwa kupata chakula kwa mwanafunzi kutwa nzima kuna madhara makubwa ikiwemo changamoto wa uelewa darasani, vidonda vya tumbo pamoja na upungufu wa lishe bora.

Sauti ya Afisa lishe halmashauri ya mji wa Bunda Lucy Mwalwayo