

11 February 2025, 6:10 pm
Aliyepotelea ziwani akiwa kwenye shughuli ya uvuvi, mwili wake umepatikana ikiwa ni siku ya tano tangu alipotoweka.
Na Edward Lucas
Kusekwa Fanuel Rufundya (31) mkazi wa kata ya Guta halmashauri ya mji wa Bunda aliyepotelea ziwani akiwa kwenye shughuli ya uvuvi, mwili wake umepatikana ikiwa ni siku ya tano tangu alipotoweka
Mwili huo umepatikana majira ya alasiri baada ya jitihada za wavuvi na wananchi katika zoezi la utafutaji tangu tarehe 7 Feb 2025 majira ya saa 2:00 asubuhi lilipotokea tukio hilo wakati marehemu na wenzake wawili wakiwa kwenye mtumbwi kwa uvu
Makongo Moni ni mmoja wa wavuvi waliokuwa na marehemu wakati wa tukio, ameiambia redio Mazingira Fm kuwa wakati wakiwa kwenye ‘mashua’ wanaelekea zilipo ndoano zao ndipo upepo ulizidi na mawimbi makali vilitokea jambo lililosababisha chombo chao kujaa maji na kuanza kuzama na katika jitihada za kujiokoa marehemu alishindwa kutokana na kukosa uzoefu wa kuogelea