Mazingira FM

Mkurugenzi TECTO community aelezea fursa za ajira kupitia utalii kanda ya ziwa

31 January 2025, 4:12 pm

Mkurugenzi wa TECTO community company Bw.Juma Elias Elias

Kanda ya ziwa inavivutio vingi vya utalii mbavyo ni fursa Katika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira nchini”

Na Catherine Msafiri,

Mkurugenzi wa TECTO community company Bw.Juma Elias Elias ameeleza kuwa Kanda ya ziwa Kuna fursa nyingi zinazowezakupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kutokana na uwepo wa vivutio vingi vya utalii ikiwemo pori la akiba kijereshi ,Hifadhi ya Taifa Serengeti na makumbusho ya baba wa Taifa mwitongo Butiama.

Ameeleza hayo alipofanya mahojiano kwenye kipindi Cha uhifadhi na utalii kinacholushwa kupitia radio Mazingira fm ambapo madam iliangazia juu ya kuvifahamu vivutio vya utalii vinavyopatikana akanda ya ziwa.

Mkurugenzi wa TECTO community company Bw.Juma Elias Elias akiwa ofisin kwake

Bw. Juma amesema kuwa kama watu wakijikita kuwekeza katika sekta ya utalii itasaidia kupunguza ukosefu wa ajira kwakua kuna fursa za biashara za kitalii kama uuzaji wa vinyago ,matunda , utengenezaji wa matenti ya kitalii,vilimo vya utalii na utalii wa kiutamaduni

Sauti ya Juma Elias Mkurugenzi wa TECTO community Company akielezea fursa za kitalii

Aidha ameshauri kuwa watu wanapaswa kujitoa kusoma masuala ya utalii na wale waliosomea wajikite katika vivutio vya Kanda ya ziwa kutasaidia kufungua shughuli za Utalii Kwa ukubwa Kanda ya ziwa

Sauti ya Juma Elias Mkurugenzi wa TECTO community Company akitoa ushauri