Mazingira FM

BUWSSA yaendelea kutanua mtandao wa maji Bunda

30 July 2024, 9:44 am

Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Bunda BUWSSA Bi, Ester Giryoma akishirikiana na wananchi katika utandazaji mabomba ya maji eneo la kata ya Bunda stoo, Picha na Mariam Mramba

Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Bunda BUWSSA Bi, Ester Giryoma awewataka wananchi kufuata utaratibu wa maunganisho mapya ya maji ili kuepuka vishoka wanaoweza kuwaibia fedha zao

Na Mariam Mramba

Wananchi wa kata ya Bunda stoo, halmashauri  ya mji wa Bunda mkoani Mara wanaelekea kuondokana na changamoto ya ukosefu wa maji iliyokuwa inawakabiri kwa muda mrefu baada ya mamlaka ya maji Bunda BUWSSA kuanza kutandaza mabomba ya maji kwenye maeneo yao.

Hayo yamesemwa na wananchi wa kata hiyo hii leo  kwenye kikao cha kukabidhi mabomba kilichoambana na zoezi la usambazaji na ulazaji mabomba katika mitaa minne ya Kata hiyo ambayo ni Kilimani,Miembeni,Idara ya maji na mtaa wa Butakale

wananchi w akata ya Bunda stoo wakiendelea na uchimbaji mtaro wa kutandaza bomba la maji, Picha na Mariam Mramba

Wakizungumza  wakati wa zoezi hilo wenyeviti wa mitaa hiyo wamekiri kuwepo kwa changamoto ya maji kwa muda mrefu ambapo wamempongeza diwani wa kata ya Bunda stoo kwa jitihada alizofanya ili kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo wanapata maji.

Diwani wa kata ya Bunda stoo Flavian Chacha Nyamageko akizungumza na wakazi wa kata yake kabla ya kuanza zoezi la utandazaji wa mabomba, Picha na Mariam Mramba

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Bunda stoo Flavian Chacha Nyamageko  amesema kuwa wahanga wakubwa wa changamoto hiyo walikuwa ni wanawakewaliokuwa wanatembea umbali mrefu kutafuta maji ambapo amewataka wananchi kutohujumu miundombinu hiyo ya maji  badala yake waitunze

sauti ya Diwani wa kata ya Bunda stoo Flavian Chacha

Naye Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Bunda BUWSSA Bi, Ester Giryoma amewatahadharisha wananchi hao kuepukana na vishoka ambao watataka kuwaunganishia maji kwa njia ya udanganyifu kwani malipo yote ya serikali yanalipwa kwa namba maalumu ya malipo (control number) na kutumia nafasi hiyo kutoa rai  kwa wananchi kutunza miradi na kuitumia kwa uadalifu, kulipa bili kwa wakati pamoja na kutoa taarifa  kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo vya wizi wa maji.

sauti ya Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Bunda BUWSSA Bi, Ester Giryoma