Mazingira FM

Wazazi wamlilia mbunge adhabu kwa wanafunzi wasiyopeleka chakula shuleni

15 July 2024, 9:00 pm

Baadhi ya wakazi wa kata ya sazira katika kutoa hoja zao kwenye mkutano wa Mbunge wa Bunda mjini

Titizo la ukosefu wa walimu wa sayansi na adhabu kwa wanafunzi ambao wazai wao wanashindwa kupeleka chakula shuleni vyatawala mkutano wa mbunge wa Bunda mjini katika kata ya Sazira.

Naa Adelinus Banenwa

Wakazi wa kata ya sazira mtaa wa ligamba wamelalamikia wanafunzi kuchapwa viboko pindi wazazi wanaposhindwa kupeleka mahindi na maharage shuleni.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara wa mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto katika kata ya Sazira wananchi hao wamesema kumekuwa na changamoto kubwa katika suala la uchangiaji chakula shuleni na walimu wamekuwa wakiwaadhibu watoto pindi mzazi asipotoa mahindi shuleni hali inayopelekea wanafunzi kuwa watoro kwa kuogopa adhabu.

sauti za wananchi
Diwani wa kata ya Sazira na mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Bunda Mhe Michael Kweka, Picha na Adelinus Banenwa

Akito ufafanuzi katika mkutano huo diwani wa kata ya Sazira na mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Bunda Mhe Michael Kweka amesema hakuna sheria yoyote inayomruhusu mwalimu kutoa adhabu kwa mwanafunzi kutokana  na mzazi kushindwa kupeleka chakula shuleni.

Wananchi wa kata ya sazira wakipata ufafanuzi kutoka kwa mbunge Maboto, Picha na Adelinus Banenwa

Amewataka wananchi kutoa taarifa kwake ikitokea mwalimu yeyote ndani ya halmashauri ya mji wa Bunda atatoa adhabu kwa mwanafunzi kutokana na mzazi kutopeleka chakula shuleni kwa sababu hilo siyo kosa la mwanafunzi.

Sauti ya Diwani Michael Kweka
Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Maboto, Picha na Adelinus Banenwa

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Bunda mjini amewaomba wakazi wa jimbo la bunda mjini kujitahidi kuchangia chakula shuleni kwa kuwa itawasaidia watoto kujifunza vizuri bila njaa.

Sauti ya mbunge Maboto