Mazingira FM

Raymond: Wafanyabiashara tumieni benki kwa usalama wa fedha

17 June 2024, 7:01 pm

Meneja Mwandamizi, Kitengo cha Biashara kutoka NMB Makao Makuu, Reynold Tony,

Wafanyabiashara msipende kutunza pesa zenu majumbani kuna hatari nyingi mfano moto, wezi n.k pelekeni benki fedha zitakuwa salama”, Raymond.

Na Adelinus Banenwa

Baadhi ya wafanyabiashara mkoani Mara wamelalamikia uwepo wa makato makubwa kwenye taasisi za kifedha hasa mabenki hali inayopelekea baadhi yao kuamua kutokutunza fedha zao kwenye taasisi hizo.

Madai hayo yametolewa mjini Musoma na wafanyabiashara hao kwenye kongamano la klabu ya wafanyabiashara wa NMB ambapo wameziomba mamlaka husika kungalia namna ya kupunguza makato hayo.

Baadhi ya wafanyabiashara na wadau wa benki Mara.

Katibu wa Chama Cha Wafugaji Wilaya ya Butiama, Peter Machugu amezitaka taasisi za fedha kukaa na serikali kuangalia namna ambavyo makato haya yanaweza yakashuka ili kuwapa nafuu wafanyabiashara na watanzania kwa ujumla.

Amesema kuwa kutokana na hali hiyo wamejikuta wakifanya biashara katika mazingira hatarishi kutokana na kulazimika kutembea na fedha kwenda minadani kwaajili ya kununua mifugo.

Sauti ya Wafanyabiashara

Meneja Mwandamizi, Kitengo cha Biashara kutoka NMB Makao Makuu, Reynold Tony amesema hali ya uwekaji wa amana kwenye taasisi za kifedha nchini bado ipo chini na kwamba kutokana na hali hiyo benki yake imekuwa ikibuni huduma mbalimbali ambazo ni rafiki ili kuhakikisha wafanyabiashara wengi wanatumia mfumo huo.

Meneja Mwandamizi, Kitengo cha Biashara kutoka NMB Makao Makuu, Reynold Tony,

Raymond amesema wamebaini wapo wafanyabiashara wengi ambao hawatumii mifumo ya kibenki jambo ambalo siyo salama kwani utunzaji wa fedha ndani una hatari nyingi ikwemo fedha kuibiwa, kuungua moto na mambo mengine.

Sauti Meneja Mwandamizi, Kitengo cha Biashara kutoka NMB Makao Makuu, Reynold Tony,