Mazingira FM

Mbunge Agness Marwa ampongeza Rais Samia kwa miradi ya maendeleo Bunda

29 May 2024, 6:37 pm

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara mhe Agness Mathew  Marwa, Picha na Adelinus Banenwa

Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais Dr Samia kwa kuleta fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa wananchi wilayani Bunda hasa kata ya Bunda stoo

Na Adelinus Banenwa

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara mhe Agness Mathew  Marwa amempongeza Rais Samia Suluhu Hasani kwa kuleta miradi mingi ya maendeleo kwa wananchi wilayani Bunda.

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara mhe Agness Mathew  Marwa, Picha na Adelinus Banenwa

Mhe Agness ameyasema hayo mara baada ya ziara yake kwenye kata ya Bunda stoo ambapo amekagua miradi ya ujenzi wa hospitali ya halmashauri ya mji wa Bunda pamoja shule ya msingi ya Bunda stoo iliyojengwa kwa mradi wa BOOST.

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara mhe Agness Mathew  Marwa, , Picha na Adelinus Banenwa

Mhe Agness amesema inatia moyo sana kuona zaidi ya shilingi bilion 2.3 hadi sasa kwenye hospitali na milioni 540 ujenzi wa shule ya msingi zinatolewa na serikali ili wananchi wapate huduma.

Sauti ya mbunge Agness Marwa
Diwani wa Bunda stoo Flaviani Chacha, Picha na Adelinus Banenwa

Kwa upande wake diwani wa Bunda stoo Flaviani Chacha amesema mbali na mafanikio mengi changamoto kubwa kwa kata ya Bunda stoo ni suala upungufu wa mtandao wa maji kutoka mamlaka ya maji Bunda pia barabara za kata zina hali mbaya kutokana na kuharibiwa na mvua.

Sauti ya Diwani Flaviani Chacha