Mazingira FM

TAKUKURU: Wananchi msishawishi watia nia kutoa rushwa

7 April 2025, 8:50 pm

Zena Kisesa mwendesha mashtaka wa TAKUKURU mkoa wa Mara

Mwananchi kushawishi mgombea au mtia nia kumpatia chochote ni kinyume na sheria ya takukuru sura ya 329 kifungu cha 15 (8)

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa wananchi kutojihusisha na vitendo vya rushwa hasa kwa kuwashawishi viongozi na watia nia kuwapatia vitu kwa lengo la kuwakubali

Wito huo umetolewa na maafisa wa TAKUKURU kutoka mkoa wa mara walipozungumza kwenye kipindi cha ufahamu wa sheria kinachorushwa hapa radio Mazingira Fm

Zena Kisesa mwendesha mashtaka wa TAKUKURU mkoa wa Mara amesema kwa namna yoyote ile mwananchi kushawishi mgombea au mtia nia kumpatia chochote ni kinyume na sheria ya TAKUKURU sura ya 329 kifungu cha 15 (8) na adhabu yake ni sawa na yule aliyetoa ama kupokea rushwa.

Zena Kisesa mwendesha mashtaka wa TAKUKURU mkoa wa Mara
Winfrida Kanyika

Naye Winfrida Kanyika afisa TAKUKURU mkoa wa Mara amesema kitendo cha wananchi  kuomba au kushawishi kupewa rushwa kinamnyima mwananchi uhuru wa kumchagua kiongozi bora hivyo wagombea wanadi sera zao na wananchi wasiwe chanzo cha kuomba rushwa,

Winfrida Kanyika