Mazingira FM

TMDA: Ukipewa dozi ya dawa maliza kuepuka UVIDA

20 November 2025, 7:55 pm

Frank Gasper Muhini, Afisa wa Mamlaka ya udhibiti wa dawa na vifaa tiba TMDA kanda ya ziwa mashariki akizungumza na wanafunzi wa chuo cha ualimu Bunda katika semina ya matumizi sahihi ya dawa

Usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa UVIDA una athari nyingi ambapo ni pamoja na gharama kubwa ya matibabu, hatari ya ugonjwa wa figo n.k

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa jamii kuhakikisha wanamaliza dozi za dawa wanazokuwa wamepewa na watoa huduma za afya pindi wanapokuwa wanaumwa.

Hayo yamesemwa na Frank Gasper Muhini, Afisa wa Mamlaka ya udhibiti wa dawa na vifaa tiba TMDA kanda ya ziwa mashariki wakati alipokuwa akitoa semina kwa wanafunzi wa chuo cha ualimu Bunda ambapo amesema ni vema mtu anapopewa dawa kutumia na mtoa huduma wa afya ahakikishe anaimaliza.

Sauti ya Frank Gasper Muhini
Frank Gasper Muhini, Afisa wa Mamlaka ya udhibiti wa dawa na vifaa tiba TMDA kanda ya ziwa mashariki akizungumza na wanafunzi wa chuo cha ualimu Bunda katika semina ya matumizi sahihi ya dawa

Frank ameongeza kuwa usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa UVIDA una athari nyingi ambapo ni pamoja na gharama kubwa ya matibabu, hatari ya ugonjwa wa figo miongoni mwa hatari zingine.

Sauti ya Frank Gasper Muhini

kwa upande wao wanafunzi wameishukuru mamlaka kwa kutoa semina na elimu kwao juu ya matumizi sahihi ya dawa hali inayoweza kusaidia kupunguza hari zinazoweza kujitokeza kutokana na usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa.

Sauti za wanafunzi