Mazingira FM

Bulaya atamatisha kampeni 2025 Bunda

25 October 2025, 8:40 pm

Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Bunda Mjini, Estar Bulaya, akiwa na kada mpya wa CCM Ezekia Wenje

Asema endapo atachaguliwa, kipaumbele chake kitakuwa ni kuinua maendeleo ya wananchi wa Bunda Mjini

Na Thomas Masalu

Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Bunda Mjini, Estar Bulaya, amehitimisha kampeni zake leo katika viwanja vya Stendi ya Zamani vilivyopo katikati ya mji wa Bunda mkoani Mara.

‎Katika hotuba yake ya kufunga kampeni, Bi. Bulaya amewashukuru wananchi wa Bunda Mjini kwa ushirikiano waliompa kipindi chote cha kampeni na kuwaomba kumpa ridhaa ya kuwa mbunge wao ili aweze kutekeleza kwa vitendo ahadi alizotoa.

Esther bulaya kulia akiwa na Ezekia Wenje katikati na Merysiana Sabuni kushoto katika mkutano wa kuhitimisha kampeni jimbo la Bunda mjini mkoani Mara

‎Ameeleza kuwa endapo atachaguliwa, kipaumbele chake kitakuwa ni kuinua maendeleo ya wananchi wa Bunda Mjini akitanabaisha kuwa changamoto kubwa ya wilaya ya bunda ni tatizo la miundombinu ya barabara ambapo amehaidi kushirikiana ana TARURA na  TANROAD kuweka miundombinu vizuri

Baadhi ya wakazi wa Bunda katika mkutano wa kampeini wa mgombea ubunge jimbo la Bunda mjini Esther Bulaya.

Pia ametaja suala la kusimamia huduma bora za afya , mikopo ya asilimia kumi  ya vikundi  miongoni mwa ahadi zingine

Sauti ya Estar Amos Bulaya,

‎Aidha , Bulaya amesema ataenda kuhakikisha mradi wa ujenzi wa stendi mpya na ya kisasa unatekelezwa, itakayoweka hadhi ya mji wa Bunda na kuchochea maendeleo ya biashara.