Mazingira FM

Jamii yatakiwa kuzingatia sheria za usalama barabarani

16 July 2025, 11:26 am

Maafisa wa polisi usalama barabarani Bunda wakitoa elimu juu ya sheria za usalama barabarani

Vipo vyanzo vya aina tatu vya ajali ambavyo ni Vyanzo vya kibinadamu, Vyanzo vya kimazingira na vyanzo vya kiufundi.

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa watumiaji wote wa barabara wilayani Bunda kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zisizo za lazima.

Hayo yamesemwa na ASP Faustin .J. Buhembere ambaye ni Mkuu wa Usalama barabarani wilaya ya Bunda wakati akizungumza na wananchi kupitia Radio Mazingira FM kwenye kipindi cha Asubuhi leo ambapo amesema ninwajibu wa watumiaji wote wa barabara kuhakikisha wanazingatia sheria za usalama barabarani.

ASP FAUSTIN .J. BUHEMBERE ambaye ni mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Bunda

ASP Buhembere amesema vipo vyanzo vya aina tatu vya ajali ambavyo ni Vyanzo vya kibinadamu, Vyanzo vya kimazingira na vyanzo vya kiufundi.

Sauti ya ASP FAUSTIN .J. BUHEMBERE ambaye ni mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Bunda.

Naye mkaguzi msaidizi wa polisi Emmanuel Joseph ambaye pia ni mkuu wa usalama barabarani msaidizi amesema kama jeshi la polisi usalama barabarani wanalo jukumu la kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya watumiaji wa barabara kupitia njia za mikutano, mashuleni, vyombo vya habari miongoni mwa njia zingine.

Mkaguzi msaidizi wa polisi Emmanuel Joseph ambaye pia ni mkuu wa usalama barabarani msaidizi.

Emmanuel amesema kundi ambalo bado linaonekana linahitaji elimu zaidi ni madereva wa pikipiki maarufu bodaboda ambalo limeonekana ni changamoto kwenye kufuata sheria za usalama barabarani.

Sauti ya mkaguzi msaidizi wa polisi Emmanuel Joseph ambaye pia ni mkuu wa usalama barabarani msaidizi