

21 March 2025, 4:24 pm
Viongozi hao wameonesha umoja na ushirikishanaji wa taarifa za miradi pindi inapopelekwa kwenye maeneo yao.
Na Adelinus Banenwa
Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bunda imewapongeza baadhi viongozi wilayani Bunda kwa utekelezaji na usimamizi wa miradi ya serikali kwenye maeneo yao.
Akizungumza katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bunda Mwenyekiti wa CCM wilaya, Abraham Mayaya Magese amesema viongozi hao wameonesha umoja na ushirikishanaji wa taarifa za miradi pindi inapopelekwa kwenye maeneo yao.
Akizungumzia mradi wa shule ya sekondari ya Nyaburundu iliyopo kata ya Ketare, Mayaya amesema kamati ya siasa baada ya kufika katika mradi huo ilikuta kuanzia viongozi wa kata mpaka wananchi wanataarifa zinazofanana kuhusu mradi huo.
Miongoni mwa waliotunukiwa hati hizo za pongezi ni pamoja an Mhe Diwani wa Kata ya Ketare Mramba Simba Nyamkinda, mkuu wa shule ya msingi Nyaburundu, Mwenyekiti wa CCM kata ya Ketare, Diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko, miongoni mwa viongozi wengine.
Wakizungumza Mara baada ya kupokea hati hizo Diwani wa kata ya Ketare Mhe Mramba Simba Nyamkinda na diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko wamesema