Mazingira FM

Diwani Ketare ambaye ni Mkurugenzi Mazingira FM atunukiwa hati ya pongezi

21 March 2025, 4:24 pm

Diwani wa kata ya Ketare Mhe Mramba Simba Nyamkinda akipokea hati ya pongezi kutoka kwa mwenyekiti wa CCM Bunda

Viongozi hao wameonesha umoja na ushirikishanaji wa taarifa za miradi pindi inapopelekwa kwenye maeneo yao.

Na Adelinus Banenwa

Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bunda imewapongeza baadhi viongozi wilayani Bunda kwa utekelezaji na usimamizi wa miradi ya serikali kwenye maeneo yao.

Akizungumza katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bunda Mwenyekiti wa CCM wilaya, Abraham Mayaya Magese amesema viongozi hao wameonesha umoja na ushirikishanaji wa taarifa za miradi pindi inapopelekwa kwenye maeneo yao.

Wajumbe wa halmashauri ya wilaya kuu CCM wilaya ya Bunda

Akizungumzia mradi wa shule ya sekondari ya Nyaburundu iliyopo kata ya Ketare, Mayaya amesema kamati ya siasa baada ya kufika katika mradi huo ilikuta kuanzia viongozi wa kata mpaka wananchi wanataarifa zinazofanana kuhusu mradi huo.

Sauti ya Mwenyekiti wa CCM wilaya, Abraham Mayaya Magese

Miongoni mwa waliotunukiwa hati hizo za pongezi ni pamoja an Mhe Diwani wa Kata ya Ketare Mramba Simba Nyamkinda, mkuu wa shule ya msingi Nyaburundu, Mwenyekiti wa CCM kata ya Ketare, Diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko, miongoni mwa viongozi wengine.

Diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko akipokea hati ya pongezi kutoka kwa mwenyekiti wa CCM Bunda

Wakizungumza Mara baada ya kupokea hati hizo Diwani wa kata ya Ketare Mhe Mramba Simba Nyamkinda na diwani wa kata ya Nyasura Magigi Samweli Kiboko wamesema

Sauti za madiwani waliotunukiwa hati za pongezi