Mazingira FM

Wananchi watakiwa kuzingatia usafi kuepuka magonjwa ya mlipuko

19 March 2025, 12:24 pm

Maafisa afya kutoka halmashauri ya mji wa Bunda

Kazi kubwa ya wataalamu ni kutoa elimu kwa jamii ili kudhibiti magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu, kichocho, miongoni mwa magonjwa mengine.

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa jamii kuzingatia usafi wa mazingira na vyakula ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko ambayo ni hatari kwa afya za wananchi,

Hayo yamesemwa na maafisa afya kutoka halmashauri ya mji wa Bunda wakati wakizungumza kupitia kipindi cha Asubuhi leo kinachorushwa na radio Mazingira Fm.

Mohamed  Mlanza mratibu wa utoaji elimu ya afya kwa jamii kutoka halmashauri ya mji wa Bunda

Mohamed  Mlanza mratibu wa utoaji elimu ya afya kwa jamii kutoka halmashauri ya mji wa Bunda amesema kazi yao kubwa kama wataalamu ni kutoa elimu kwa jamii ili kudhibiti magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu, kichocho, miongoni mwa magonjwa mengine,

Akizungumzia ugonjwa wa homa ya nyani (M-POX) Mlanza amesema ugonjwa huo umeshatangazwa na serikali kwamba upo hivyo ni jukumu la wananchi kuchukua tahadhari endapo wataona dalili za ugonjwa huo ambazo ni pamoja na vipere sehemu za usoni, miguuni, mikononi , homa , maumivu ya kichwa miongoni mwa dalili zingine.

Sauti ya Mohamed  Mlanza mratibu wa utoaji elimu ya afya kwa jamii kutoka halmashauri ya mji wa Bunda
Amani Mashauri Jumbula, afisa afya halmashauri ya mji wa Bunda

Kwa upande wake Amani Mashauri Jumbula, afisa afya halmashauri ya mji wa Bunda amesema mbali na elimu inayotolewa lakini jukumu kubwa lipo kwa wananchi kuzingatia usafi hasa katika magonjwa kama kipindupindu chanzo chake ni uchafu hasa pale mtu anapokula chakula chenye vimelea vya wadudu wa kipindupindu ambao msingi wake ni kinyesi .

Ametoa wito kwa jamii kuzingatia kanuni zote za afya ikiwemo kunawa mokono, kuwa na vyoo bora , kuepuka kula vyakula ambavyo nivyabaridi miongoni mwa tahadhari zingine.

Sauti ya Amani Mashauri Jumbula, afisa afya halmashauri ya mji wa Bunda