Mazingira FM

Radio Mazingira FM yapongezwa kwa utendaji kazi mzuri

14 February 2025, 12:46 pm

Mkuu wa wilaya ya Musoma Juma Chikoka alipokuwa akizungumzia siku ya radio,(picha na Shomari)

Mkuu huyo wa wilaya ya Musoma amekipongeza kituo cha redio cha Mazingira Fm cha mjini Bunda kwa kazi nzuri za kuendelea kuwafikishia wananchi taarifa mbalimbali.

Na.Shomari Binda

Katika kuadhimisha siku ya radio duniani jamii imetakiwa kufatilia matangazo yake ili kuweza kupata taarifa mbalimbali zikiwemo za utekelezaji wa miradi ya serikali.

Kauli hiyo imetolewa februari 13,2025 na mkuu wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka alipokuwa akiizungumzia siku hiyo.

Amesema redio ni chombo muhimu na kinachopaswa kufatiliwa hivyo wananchi wanakumbushwa kufatilia matangazo yanayotolewa

Chikoko amesema ipo miradi inayotekelezwa na serikali katika Wilaya ya Musoma na maeneo mengine ya nchi na moja ya vyanzo vya kupata taarifa ni kupitia redio

Mkuu huyo wa Wilaya ya Musoma amekipongeza kituo cha redio cha Mazingira Fm cha mjini Bunda kwa kazi nzuri za kuendelea kuwafikishia wananchi taarifa mbalimbali.

Chikoka kupitia siku hii ya redio duniani amewapongeza watangazaji wa Mazingira Fm kwa kazi wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa