Mazingira FM

Bunda: Shule kukosa mwalimu wa kike, DC atoa maagizo mazito

12 February 2025, 10:53 pm

Dr Vicent Naano Anney, DC Bunda akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya wilaya (Picha na Edward Lucas)

Kati ya walimu 350 waliopo halmashauri ya wilaya ya Bunda walimu wa kike ni 45 pekee.

Na Edward Lucas

Kutokana na kilio cha kukosa mwalimu wa kike shule ya sekondari Tirina, mkuu wa wilaya ya Bunda, Dr Vicent Naano Anney amempa siku moja mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo awe amempa barua ya kuonesha mwalimu amepelekwa katika shule hiyo

Naano ametoa maagizo hayo leo kupitia mkutano wa baraza la madiwani kupokea taarifa mbalimbali ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025 katika halmashauri ya wilaya ya Bunda

George Stanley Mbilinyi, DED halmashauri ya wilaya ya Bunda akiwa katika mkutano wa Baraza la Madiwani (Picha na Edward Lucas)

Awali akizungumzia changamoto hiyo diwani wa kata ya Mugeta, Mganga Jongora amesema shule ya sekondari Tirina ina wanafunzi wa kike na wa kiume lakini toka shule hiyo ifunguliwe haina mwalimu wa kike jambo linalosababisha wanafunzi wa kike wakose mtu wa kumfikishie changamoto zao

Sauti ya Mganga Jongora, Diwani wa Mugeta

Katika mahojiano na Mazingira Fm, Kaimu Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri ya wilaya ya Bunda, Nambua Godfrey Semlugu amekiri kuwepo changamoto ya uhaba wa walimu wa kike kwani kati ya walimu 350 wa kike ni 45 pekee.

Sauti ya Nambua G. Semlugu