Mazingira FM

Serikali kulipa riba ya asilimia 7 Nyatwali kwa kuchelewesha fidia zao

5 September 2024, 8:28 pm

Mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi akisoma mfano wa hundi ya fedha baada ya kukabidhi kwa wakazi wa Nyatwali ikiwa ni uzinduzi wa malipo ya fidia kwa wakazi hao, Picha na Adelinus Banenwa

Zoezi la ulipaji fidia likiwa limefunguliwa rsmi kwa wakazi wa kata ya Nyatwali, mbunge wa Bunda mjini ataka mambo kadhaa yazingatiwe ikiwemo riba ya asilimia saba kutokana na kucheleweshwa kwa fidia zao

Na Adelinus Banenwa

Serikali imeridhia kulipa asilimia saba kama riba ya kuchelewesha ulipaji wa fidia kwa wakazi wa kata ya Nyatwali.

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Mara Mhe Kanal Evans Mtambi wakati wa zoezi la uzinduzi waulipaji wa fidia kwa wakazi wa Nyatwali leo 5 Sept 2024.

Mhe Mbunge wab Jimbo la Bunda mjini Robert Chacha Maboto akiwasilisha baadhi ya hoja za wakazi wa Nyatwali ambazo hazijapatiwa majibu, Picha na Adelinus Banenwa

Awali akiwasilisha baadhi ya hoja za wakazi wa Nyatwali Mhe mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto amesema pamoja za zoezi la ulipaji wa fidia  kuzinduliwa yapo malalamiko ya wananchi ambayo bado hayajafanyiwa kazi.

baadhi ya wakazi wa Nyatwali wakisikiliza viongozi katika uzinduzi wa ulipaji wa fidia kwa wakazi hao, Picha na Adelinus Banenwa

Mhe Robert Chacha Maboto ameitaka serikali kutoa majibu ya maswali ya wananchi wa kata ya Nyatwari hasa asilimia 7 ambayo ni riba ya kucheleweshwa kwa fidia yao, Eneo la Mjapani, haki ya kuandikishwa kupiga kura miongoni mwa maswali mengine.

Sauti ya mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto
Mkuu wa mkoa wa Mara Mhe Kanal Evans Mtambi akitoa ufafnuzi wa baadhi ya masuala katika hafla ya uzinduzi wa ulipaji fidia kwa wakazi wa kata ya nyatwali, Picha na Adelinus Banenwa

Akijibu hoja hizo  Kanal Mtambi ameelekeza maeneo yaliyoachwa bila kupimwa likiwemo eneo la magwata, eneo la mjapani na maeneo ya watu wengine yaliyobaki kuhakikisha yote yanapimwa

sauti ya mkuu wa mkoa wa Mara Mhe Kanal Evans Mtambi

Sambamba na hilo Mhe Mtambi ameridhia wakazi hao wa Nyatwali kuchukua sehemu ya vifaa vinavyotoka kwenye nyumba ikiwa ni pamoja na mabati,  tofali  miongoni mwa mali zingine.

sauti ya mkuu wa mkoa wa Mara Mhe Kanal Evans Mtambi