Mazingira FM

Wanufaika TASAF Bunda walia ucheleweshwaji fedha zao

10 May 2023, 10:56 am

Wito umetolewa kwa walengwa wa TASAF wilaya ya Bunda kuudhulia warsha za mafunzo ilikuwa na uelewa kuhusu mambo mbalimbali yanayohusu malipo kwa familia hizo

hayo yamesemwa na afisa ufuatiliaji TASAF wilayani Bunda Alex Kumwalu alipokuwa akizungumza na wanufaika wa TASAF kata ya Bunda Stoo  katika kujibu changamoto mbalimbali zilizoelezwa na wanufaika hao.

ALEX KUMWALU AKIWASIKILIZA WANUFIKA WA TASAF BUNSA STOO

Kumwalu amesema tatizo kubwa kwa wanufaika pindi wanapokwenda kwenye warsha hizo hawafuatilii yale mafundisho na elimu wanayopewa badala yake wanawaza kupata fedha na kuondoka jambo linaloleta ugumu kwa waratibu maana katika mpango wa kuzinusuru kaya maskini kuna ruzuku tofauti kulingana na kaya yenyewe

kwa upande wao walengwa wa TASAF wamesema tatizo kubwa ni ucheleweshwaji wa fedha hizo maana mara ya mwisho ililipwa ile ya mwezi  Nov na Dec mwaka jana ambayo waliipata mwezi wa pili mwaka huu mpaka sasa hawajapta fedha yao sasa yapata mwezi wa tano

aidha changamoto nyingine iliyobainishwa ni upungufu wa vifaa vya kazi katika mpango wa ajira za muda mfano kama gunboot, groves, majembe miongoni mwa vifaa vingine

Flavian Chacha – Diwani

Naye diwani wa kata ya Bunda stoo Mhe Flavian Chacha amesema mara kadhaa amepokea malalamiko kutoka kwa wananchi wake hao ambao ni walengwa juu ya kucheleweshewa malipo yao jambo lililomsukuma kuitisha kikao hicho ili kuwakutanisha walengwa na waratibu wa TASAF ili kupata majibu ya changamoto zao

Hata hivyo ameshukuru mpango wa ajira za muda za TASAF maana zimeleta mabadiriko katika barabara zilizofunguliwa na wanufaika hao.