Baraka FM
Baraka FM
6 June 2024, 15:27

Wakati mtaani malalamiko yakiendelea kuwa mengi kuhusiana na kupanda kwa vocha wananchi wanapaswa kutoa taarifa kwa wahusika na wasimamizi wa mawasiliano nchini.
Na Hobokela Lwinga
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imewataka wauzaji wa vocha kuacha kupandisha bei za vocha kiholela na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.
Wito huo umetolewa na Meneja wa TCRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bw. Bonface Shoo wakati akizungumza na kituo hiki katika kipindi cha jarida kinachorushwa na kituo cha redio Baraka FM.

Shoo amesema waliopandisha vocha sio makampuni bali ni mawakala ambao wameamua kuvunja kanuni na sheria .
Aidha meneja huyo amewataka wananchi wanaokumbana na kero hiyo kutoa taarifa ili kuweza kuwabaini wauzaji wanaouza kinyume na utaratibu sambamba na kuwataka watumiaji wavocha kutumia huduma za kifedha kununua vifurushi ili kuondokana na kero hiyo.