Baraka FM

Wanawake Block D Ilomba watembelea gereza la Rwanda,Mbeya

3 March 2025, 10:08

Baadhi ya wanachama Umoja wa kina mama mtaa wa Block D Ilomba(picha na Ezra Mwilwa)

Katika kuadhimisha kilele cha siku ya mwanamke Duniani wanawake mkoani Mbeya watumia nafasi hiyo kuwatembelea wahitaji mbalimbli.

Na Ezra Mwilwa

Kuelekea siku ya mwanamke duniani Umoja wa kina mama mtaa wa Block D Ilomba wametembelea gereza la Ruanda upande wa wanawake kwa lengo la kuwafariji na kuwapelelea baadhi ya mahitaji.

Makamu mwenyekiti wa umoja huo Neema Kibona amesema katika kuadhimisha siku ya mwanamke Duniani wamekua na utaratibu wa kutembelea wahitaji.

Baadhi ya wanawake walio farika Gereza la Rwanda kutoa msaada kwa wafungwa wanawake(picha na Ezra Mwilwa)

Kibona amewawaomba wanawake wote kunitumia siku hiyo kusaidia wahitaji waliopo maeneo tofautitofauti.

naye Askari Mkaguzi msaidizi Juliana Akioo kutoka gereza la Rwanda amewashukuru wanawake hao kwakutambua uhitaji wawanawake wafungwa gerezani.

Askari Mkaguzi msaidizi Juliana Akioo kutoka gereza la Rwanda(picha na Ezra Mwilwa)

Siku ya mwanamke Duniani imekua ikiadhimisha Kila mwaka ifikapo mwezi Machi tarehe 8