Baraka FM
Baraka FM
12 May 2026, 08:07

kufuatia changamoto ya utoroshaji wa zao la pareto kwa baadhi ya watu wanao daiwa kuwa mawakala serikali imejipanga kudhibiti changamoto hiyo.
Na Ezra Mwilwa
Mawakala wa ununuzi wa zao la pareto wametakiwa kuzingatia taratibu na njia bora za ununuzi wa zao hilo, pamoja na kutumia mizani iliyokaguliwa rasmi ili kuhakikisha haki na uwazi kwa wakulima.

Wito huo umetolewa afisa kilimo wa wilaya za Mbeya Cathibeti Mwinuka amesisitiza umuhimu wa kufuata sheria na kanuni za ununuzi wa mazao ili kulinda maslahi ya wakulima na kuongeza ufanisi katika biashara ya pareto.
Naye Rachel Ndaro kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo Uyole (TARI Uyole)amesema kwa sasa bado kuna changamoto ya upatikanaji wa mbegu rasmi za zao la pareto, huku akibainisha kuwa watafiti wapo katika hatua za mwisho za kupata mbegu bora na rasmi zitakazosaidia kuongeza uzalishaji na ubora wa zao hilo.

Aidha viongozi wa kampuni ya PCT Edesius Mbegu pamoja na Misa Malubalo, wameeleza changamoto mbalimbali zinazoikabili kampuni hiyo katika shughuli za ununuzi huku wakieleza matarajio yao ya kuboresha huduma na kuongeza mafanikio katika msimu ujao.