Baraka FM
Mbunge Sikonge Tabora aipongeza halmashauri ya Rungwe Mbeya
12 December 2023, 19:23
Na mwandishi wetu,Rungwe Mbeya
Mheshimiwa Joseph Kakunda Mbunge wa Jimbo la Sikonge Mkoa wa Tabora ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Rungwe kwa Kuzalisha zaidi ya lita za maziwa million 44 kwa mwaka hatua iliyoongeza kipato cha wananchi sambamba na uboreshaji wa Maisha yao.
Pongezi hizo amezitoa leo tarehe 12.12.2023 wakati wa mawasilisho ya namna Wilaya ya Rungwe ilivyofanikiwa katika uboreshaji wa mifugo na ukusanyaji wa mapato ya serikali.
Viongozi mbalimbali kutoka Wilaya ya Sikonge wamefanya ziara katika wilaya ya Rungwe lengo likiwa ni kujifunza namna bora ya Ukusanyaji wa mapato, Usimamizi wa miradi ya Maendeleo, sekta ya Kilimo na Mifugo, elimu, Viwanda pamoja na Utalii.