Baraka FM

Mahongole wadai maendeleo yao yameletwa na diwani

10 July 2025, 16:01

Diwani wa kata ya Mahongole anayemaliza muda wake mhe. Patrick Mwaisoba(kushoto)akiwa na mwananchi wake Erica Mbogela(kulia)-picha na Hobokela Lwinga

Kwenye maisha usiwe mtu wa kujisifu badala yake acha kazi yako na bidii yako ikutambulishe kwa watu,ndio hapo utasifiwa na wanao ona.

Na Hobokela Lwinga

Wananchi katika kijiji cha Nsonyanga A kata ya Mahongole wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wameishukru serikali kupitia kwa diwani wa kata hiyo Patrick Mwaisoba kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

‎Wakizungumza na kituo hiki baada ya kutembelewa katika Kijiji cha Nsonyanga wananchi hao wamesema diwani wao amekuwa chachu kubwa ya maendeleo 

‎Erica Mbogela ni mwananchi,amesema diwani wao huyo katika uongozi wake  imefanikisha ujenzi wa shule ya Sekondari Shamlindima  hali iliyosaidia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu katika shule ya Sekondari Ruiwa ‎Iliyopo nje ya kijiji chao.

‎Erica Mbogela mwananchi katika Kijiji cha Nsonyanga kata ya Mahongole Wilaya ya Mbarali (picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya ‎Erica Mbogela

‎Nae mwenyekiti wa Kijiji cha Nsonyanga A Gasper kalinga ameishukru serikali kwa kutoa ushirikiano wa kufanikisha maendeleo kupitia uongozi wao katika sekta mbalimbali za elimu,afya na maji.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsonyanga A Gasper kalinga(Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mwenyekiti wa Kijiji cha Nsonyanga A Gasper kalinga

‎Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya shule ya Sekondari Shamlindima,ambaye pia ni mchungaji wa ushirika wa Nsonyanga Amos Mwangole amesema wao kama viongozi wa dini wamekuwa chachu ya ujenzi wa Shule mpya tangu ujenzi wake kuanza hadi ulipofikia sasa.

Mjumbe wa kamati ya shule ya Sekondari Shamlindima,ambaye pia ni mchungaji wa ushirika wa Nsonyanga Amos Mwangole (picha na Hobokela Lwinga)
sauti ya Mjumbe wa kamati ya shule ya Sekondari Shamlindima,ambaye pia ni mchungaji wa ushirika wa Nsonyanga Amos Mwangole

‎Hata hivyo kituo kimetafuta Diwani huyo wa kata ya Mahongole anayemaliza muda wake mhe. Patrick Mwaisoba amesema mafanikio yake kwenye uongozi wake yametokana na ushirikiano anaoupata kutoka kwa wananchi

Diwani wa kata ya Mahongole anayemaliza muda wake mhe. Patrick Mwaisoba(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Diwani wa kata ya Mahongole anayemaliza muda wake mhe. Patrick Mwaisoba