Baraka FM

Wadiakonia Moravian wajengewa uwezo kuhudumia watu wenye uhitaji

25 September 2025, 15:50

Baadhi ya washiriki wa semina ya udiakonia wilaya ya Mbalizi (Picha na Hobokela Lwinga)

Kusaidia watu wenye mahitaji ni sehemu ya maagizo ya Mungu kwenye maandiko Matakatifu yaani Biblia Yakobo 1:27 inasema “Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.”

‎Na Hobokela Lwinga
‎Viongozi wa udiakonia wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi wametakiwa kufanya kazi ya udiakonia kwa weledi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa jamii na kusaidia makundi ya watu wasiojiweza.

‎Rai hiyo imetolewa na mkufunzi wa semina za Udiakonia Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Lulu Mpenja wakati akifundisha semina ya udiakonia kwa viongozi wa udiakonia wilaya ya Mbalizi iliyofanyika katika ushirika wa Mlima reli.

Sauti ya mkufunzi wa semina za Udiakonia Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Lulu Mpenja

‎Katika hatua nyingine mkufunzi huyo amesema wajibu wa mdiakonia ni kuwezesha kuwajengea uwezo watu wenye uhitaji mbalimbali namna ya kujitegemea katika maisha yao.

Sauti ya mkufunzi wa semina za Udiakonia Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Lulu Mpenja
Mkufunzi wa semina za Udiakonia Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Lulu Mpenja(picha na Hobokela Lwinga)

‎Akifundisha somo la upimaji wa VVU na faida zake Juliana Willa amewakumbusha washiriki kutokuwanyanyapa wagonjwa wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi huku akitaja faida ya kupima kuwa ni kujua afya yako na namna ya kuishi.

Sauti ya Mkufunzi wa somo la upimaji wa VVU na faida zake Juliana Willa
Mkufunzi somo la upimaji wa VVU na faida zake Juliana Willa(picha na Hobokela Lwinga)

‎Kwa upande wake mwenyekiti wa kanisa la Moravian Tanzania wilaya ya Mbalizi mch.Erica Mwanijembe amewataka viongozi hao kutumia nafasi ya elimu waliyoipata kuhamasisha wakristo kwenye shirika zao kushiriki vyema kushiriki sikukuu ya udiakonia inayotarajia kufanyika October 12,mwaka huu.

Sauti ya mwenyekiti wa kanisa la Moravian Tanzania wilaya ya Mbalizi mch.Erica Mwanijembe
Mwenyekiti wa kanisa la Moravian Tanzania wilaya ya Mbalizi mch.Erica Mwanijembe(picha na Hobokela Lwinga)

‎Baadhi ya washiriki wamelishukru kanisa kupitia idara ya udiakonia kwa kuendelea kutoa elimu ambayo inawawezesha kufanya kazi yao ya udiakonia kwa weledi.

Sauti za baadhi‎ ya washiriki
Mkufunzi wa semina za Udiakonia Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Lulu Mpenja akiendelea kutoa elimu ya maambukizi ya VVU na kujikinga (picha na Hobokela Lwinga)

Ikumbukwe kuwa semina zote zinatolewa na idara ya udiakonia katika Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi zinafadhiliwa na shirika la mission 21.