Baraka FM

Watu wenye ulemavu watakiwa kutumia fursa za elimu ya ujasiriamali kujiinua kiuchumi

17 June 2025, 19:06

Wachungaji na wageni wenigine wakiongozwa na Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Robert Pangani (wa tano kulia)na kutoka kushoto wa tano ni mgeni rasmi bw.Raphael Shitindi halmashauri ya wilaya ya Mbarali, ambaye ni afisa mazingira wilaya ya Mbarali(Picha na Hobokela Lwinga)

Wadau na taasisi mbalimbali  wameombwa kutowatenga wahitaji badala yake wanatakiwa kujenga utamaduni wa kuwatembelea na kuwasaidia wahitaji misaada mbalimbali kwani kufanya hivyo ni sadaka na  thawabu mbele za Mungu.

‎Na Hobokela Lwinga

Watu wenye ulemavu wametakiwa kutumia fursa za elimu ya ujariamali wanazozipata ilikuweza kujiinua kiuchumi hali itakayowaondolea utegemezi.

Rai hiyo imetolewa na Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Robert Pangani wakati akifunga semina ya watu wenye ulemavu katika halmashauri ya wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya iliyoandaliwa na idara ya udiakonia katika kanisa hilo iliyofadhiliwa na mission 21.

Askofu Pangani amesema kuwa mlemavu hakuondoi uwajibikaji wa kuzalisha mali.

Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Robert Pangani(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Robert Pangani

Kwa upande wake mwakilishi wa serikali katika halmashauri ya wilaya ya Mbarali, ambaye ni afisa mazingira bw.Raphael Shitindi amesema serikali inaendelea kuweka mazingira Mazuri kwa watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na fursa za mikopo isiyo na riba ya asilimia kumi inayotolewa na halmashauri.

Sauti ya mwakilishi wa serikali katika halmashauri ya wilaya ya Mbarali, ambaye ni afisa mazingira bw.Raphael Shitindi

Aidha akitoa taarifa Mbeya ya wageni na washiriki, Katibu idara ya udiakonia kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi bw.Eliud Mahenge amesema lengo la kuanda mafunzo hayo kwa watu wenye ulemavu ni kuwawezesha kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye jamii.

Katibu idara ya udiakonia kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi bw.Eliud Mahenge(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Katibu idara ya udiakonia kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi bw.Eliud Mahenge

Hata hivyo akizungumza mwakilishi wa shirika la mission 21 Adriane sweetman amesema wataendelea kutoa ushirikiano kwa kanisa katika kuratibu uwezeshaji wa makundi ya watu wenye ulemavu kwani lengo lao ni kuwawezesha watu hao kiuchumi na kiafya.

Mwakilishi wa shirika la mission 21 nchini Tanzania Adriane sweetman(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mwakilishi wa shirika la mission 21 Adriane sweetman

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamewashukru wafadhiri likiwemo kanisa la Moravian Jimbo la kusini magharibi, mission 21 kwa kuona umuhimu wa kufanya mafunzo kwa wetu wenye ulemavu.

‎Katika ufungaji wa mafunzo hayo Baraka fm radio imetunukiwa cheti cha heshima kwa kutambua mchango wa uandaaji wa maudhui ya kupigania haki za watu wenye ulemavu kilichotolewa na Shirika la Tanzania Joy Women Entrepreneurship for the Deaf (FUWAVITA) lenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam.

Cheti cha heshima kilichotolewa na na Shirika la Tanzania Joy Women Entrepreneurship for the Deaf (FUWAVITA)