Baraka FM

Udiakonia Moravian yawafikia walezi, wazazi kituo cha kulea yatima Amani Nsalaga

9 June 2025, 15:09

Baadhi ya washiriki wa semina ya udiakonia katika kituo cha kulea watoto yatima Nsalaga Mbeya(picha na Hobokela Lwinga)

Kanisa la Moravian Jimbo la kusini magharibi limeendelea kutoa elimu kwenye taasisi na idara zake kuhusu umuhimu wa kufanya matendo ya huruma yaani udiakonia.‎‎

Na Hobokela Lwinga ‎‎

Walezi na wahudumu wa watoto katika vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima na watoto wenye mahitaji maalumu wamekumbushwa wajibu wao katika kuwalea watoto kwenye misingi ya neno la Mungu‎‎.

Rai hiyo imetolewa na makamu mwenyekiti kanisa la Moraviani Tanzania jimbo la kusini magharibi Asulumenye Mwahalende wakati akifungua semina ya udiakonia yenye lengo la kutoa Elimu ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi, Semina hiyo imefanyika katika kituo cha watoto ya tima Cha  Amani Nsalaga kilichopo jijini Mbeya.‎‎

Makamu mwenyekiti kanisa la Moravian Tanzania jimbo la kusini magharibi Asulumenye Mwahalende(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya makamu mwenyekiti kanisa la Moravian Tanzania jimbo la kusini magharibi Asulumenye Mwahalende

Nae  katibu wa Idara ya udiakonia katika kanisani la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Eliudy  Mahenge Ameeleza lengo la  Idara ya Udiakonia  kuwa ni kutoa huduma kwa wahitaji.‎‎

katibu wa Idara ya udiakonia katika kanisani la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Eliudy  Mahenge(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti katibu wa Idara ya udiakonia katika kanisani la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Eliudy  Mahenge

Aidha Afisa Afya Idara ya Udiakonia wa kanisa la Moraviani Tanzania jimbo la kusini magharibi Emmanuel Angetile Ameitaka jamii kutokuwabagua watoto kwani watoto hao ni msaada kwa ajili ya wakati ujao.‎‎

Afisa afya Idara ya Udiakonia wa kanisa la Moraviani Tanzania jimbo la kusini magharibi Emmanuel Angetile(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya afisa afya Idara ya Udiakonia wa kanisa la Moravian Tanzania jimbo la kusini magharibi Emmanuel Angetile

Hata hivyo mkufunzi katika semina hiyo Ambaye ni mhudumu wa afya nasihi  Juliana willa  amewakumbusha wazazi na walezi wa watoto kutoa malezi Bora kwa watoto wao ili kuepukana na makundi rika.‎‎

Sauti ya mkufunzi wa semina na mhudumu wa afya nasihi  Juliana willa

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa semina hiyo,msimamizi wa kituo cha watoto yatima Amani Nsalaga Mch.Elizabeth Nampasa amesema elimu waliyoipata itakuwa msaada kwao kwa ajili ya kutoa malezi Bora kwa watoto wanaowahudumia.‎

Msimamizi wa kituo cha watoto yatima Amani Nsalaga Mch.Elizabeth Nampasa(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya msimamizi wa kituo cha watoto yatima Amani Nsalaga Mch.Elizabeth Nampasa