Baraka FM

Wanahabari wapigwa msasa matumizi ya mtandao wa radio jamii

26 May 2025, 15:31

Afisa Tehama Redio jamii Amua Rushita akitoa mafunzo kwa wana habari. Picha na mwandishi wetu

Kutokana na uwepo wa uzalishaji maudhui mbalimbali katika mitandao ya kijamii waandishi wa habari wametakiwa kutumia taaluma Zao kuelimisha jamii

Na Ezra Mwilwa

Mafunzo hayo yaliyo andaliwa na mtandao wa Radio Jamii (TADIO) yamefanyika katika ukumbi wa hotel ya Mdope jijini mbeya Amua Rushita ambaye ni Afisa Tehama wa mtandao wa radio jamii amesema nimuhimu sana Redio kutumia mfumo wa radio jamii ili kusaidia usikivu katika maeneo mbalimbali ulimwenguni.

Wanahabari kutoka mikoa mbalimbli wa kiendelea na mafunzo Mbeya. Picha na Mwandishi wetu

Mratibu wa mafunzo hayo kutoka TADIO Fatuma Mahendeka amesema wameanda mafunzo hayo kwa siku mbili ili kukumbushana namna ya uandishi Bora wa habari za kuelimisha jamnii nzima.

mratibu wa mafunzo hayo kutoka TADIO Fatuma Mahendeka. Picha na Ezra Mwilwa

Nao baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki mafunzo hayo wamesema mtandao wa radio jamii tangu kuanzishwa kwake umekua na msaada mkubwa hasa katika kuifikia jamii