Baraka FM

Moravian Nsonyanga yafanya maombi kuelekea uchaguzi mkuu

19 May 2025, 16:52

Ni jukumu la kila mwananchi kuombea taifa ili liendelee kuwa na amani na katika hilo kila mtu anaowajibu wakulinda amani ya nchi.

Na Hobokela Lwinga

Waumini Wakanisa La Moravian Tanzania Ushirika Wa Nsonyanga Uliopo Halmashauri Ya Mbeya Wamefanya Ibada Ya Kuliombea Taifa Kuelekea Uchaguzi Mkuu October,2025.

Ibada Hiyo Imeongozwa Na Mchungaji Wa Ushrika Wa Nsonyanga Amosi Mwangole Huku Ikihudhuliwa Na Viongozi Wa Serikali Wakiongozwa Na Diwani Wa Kata Ya Mahongole Mhe.patrick Mwaisoba.

Akizungumzia Umuhimu Wa Kuombea Taifa Mchungaji Amesema kanisa kazi yake ni kuomba nyakati zote pia amesistiza uwepo wa uchaguzi wa haki na amani.

Aidha mchungaji Mwangole amewataka wananchi kwenda kupiga kula ya kumchagua kiongozi wanayemtaka ili aweze kuwaongoza.

Baadhi ya waumini kanisa la Moravian ushirika wa Nsonyanga Mbarali Mbeya (picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Mchungaji Wa Ushrika Wa Nsonyanga Amosi Mwangole

Nae Diwani Wa Kata Ya Mahongole halmashauri ya wilaya ya Mbarali Mhe. Patrick Mwaisoba ameomba Kanisa Liendelee Kuliombea Taifa Kwani Kila Mamlaka Inayongoza Taifa lolote duniani Inatoka Kwa Mungu huku akilishukru kanisa kwa kutambua umuhimu wa kuliombea taifa.

Diwani Wa Kata Ya Mahongole halmashauri ya wilaya ya Mbarali Mhe. Patrick Mwaisoba(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Diwani Wa Kata Ya Mahongole halmashauri ya wilaya ya Mbarali Mhe. Patrick Mwaisoba

Baadhi Ya Waumini Walioshiriki Ibada Hiyo Wamesema wanamuomba mungu awarejeshee viongozi wote waliofanya kazi vizuri katika utendaji wao uchaguzi ujao mwaka huu 2025.

Mchungaji Amos Mwangole akimpa zawadi ya kuku diwani wa kata ya Mahongole Mhe.Patrick Mwaisoba(kulia)picha na Hobokela Lwinga
Sauti ya mmoja wa waumini ushirika wa Nsonyanga