Baraka FM

RC Mbeya aitembelea shule ya Holly Land Chunya

10 February 2025, 22:41

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Holly Land

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Zuberi Homera ametembelea shule ya mchepuo wa Kiingereza ya Holly Land iliyopo Mamlaka ya Mji Mdogo wa Makongolosi Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya.

Lengo la kutembelea shule hiyo ni kuipongeza kwa matokeo mazuri tangu kuanzishwa kwake na uwekezaji mkubwa wa Lawena Nsonda(Baba Mzazi).

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Holly Land chunya (picha na Ezekiel Kamanga)

Aidha amewataka wazazi Mkoani Mbeya kuwapeleka watoto shuleni hapo badala ya kuwapeleka mbali kwani shule ina huduma nzuri na malezi mazuri.

Kwa upande wake Lawena Nsonda (Baba Mzazi) ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa kwa wawekezaji nchini wakiwemo wamiliki wa Shule.

Mkurugenzi wa Shule ya Holly Land kushoto(picha na Ezekiel Kamanga)

Shule ya Holly Land ni moja ya shule bora zinazofa vema Kiwilaya,Kimkoa na Kitaifa.