Baraka FM

Viongozi watakiwa kuhimiza michezo kuchochea ajira kwa vijana

30 July 2024, 18:40

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Noah Mwakisu (kushoto) akimpongeza diwani wa kata ya Shizuvi Noah Mwashibanda (kulia) kwa kuandaa ligi ya mpira katani kwake (Picha na Hobokela Lwinga)

Michezo ni afya na ndiyo sababu wataalam wa afya wamekuwa wakihimizwa ufanyaji wa mazoezi kwani husaidia kujiepusha na magonjwa yasiyoambukizwa.

Na Hobokela Lwinga, Mbeya

Viongozi mbalimbali wametakiwa kulipa kipaumbele suala la michezo kwenye maeneo yao hali itakayoimarisha ushirikiano katika kuchochea maendeleo ya mtu mmoja na taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na mjumbe wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi Noah Mwakisu wakati akimwakilisha mjumbe wa kamati ya CCM taifa Ndg. Ndele Mwaselela katika ufungaji wa ligi ya mpira wa miguu Mwashibanda Cup iliyofanyika kata ya Shizuvi halmashauri ya Mbeya.

Ndugu Mwakisu amesema mpira umetoa ajira nyingi kwa vijana hivyo kila mtu anapaswa kuithamini sekta hiyo ya michezo.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Noah Mwakisu(Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Noah Mwakisu

Kwa upande wake diwani wa kata ya Shizuvi ambaye ndiye mwandaaji wa mashindano hayo Noah Mwashibanda amesema wanathamini michezo kwenye kata yao kwani imewakutanisha watu mbalimbali huku akisema mshindi wa kwanza amepata zawadi ya ng’ombe.

Diwani wa kata ya Shizuvi ambaye ndiye mwandaaji wa mashindano hayo Noah Mwashibanda(Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya diwani wa kata ya Shizuvi ambaye ndiye mwandaaji wa mashindano hayo Noah Mwashibanda

Hata hivyo mratibu wa mashindano hayo Patrick Mwayinga amesema vilabu vimeonyesha uwezo mkubwa kwani time zingine zimefanya usajili wachezaji kutoka nje ya nchi.

Mratibu wa mashindano hayo Patrick Mwayinga(Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mratibu wa mashindano hayo Patrick Mwayinga

Baadhi ya wachezaji walioshiriki ligi hiyo wamemshukru diwani wao kwa kuwaunganisha kupitia michezo kwenye kata yao.

Sauti za baadhi ya washiriki wa mashindano

Mashindano ya Mwashibanda cup yametamatika huku ikijumuisha timu 11 zote zikiwa ni timu zinatoka ndani ya kata ya Shizuvi.