Baraka FM

Wakristo Mbeya wafanya maombi maeneo ya ajali zinakotokea mara kwa mara

14 July 2024, 11:37

Kutokana na ajali za mara kwa mara mkoani Mbeya zimewafanya wakristo kufanya ibada ya maombezi kukomesha matukio hayo.

Na Deus Mellah

Jukwaa la wakristo wa madhehebu mbalimbali mkoani  Mbeya  wamefanya maandamano ya amani  na kuombea maeneo ambayo ajali zimekuwa zikitokea  mara kwa mara ikiwa ni pamoja na kuombea eneo la mteremko wa mlima Iwambi na mteremko wa Mbembela.

Baada ya maombi hayo kufanyika ibada ilihitimishwa katika kanisa la Moravian jimbo la Kusini Magharibi ushirika wa Iyunga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na serikali.

Akizungumza katika tukio hilo askofu wa kanisa la Moravian Tanzania jimbo la Kusini Magharibi Mch Robert Pangani ameishukuru serikali kwa kuwaunga mkono katika tukio hilo huku akiwaasa wakristo kuendelea kuiunga mkono serikali katika shughuli mbalimbali za maaendeleo.

Sauti ya askofu Robert Pangani

Askofu Robert Pangani amewaomba wakristo kuendelea kuombea majanga mbalimbali yasiendelee kutokea nchini yakiwemo mauaji ya watu wenye ulemavu, unyanyasaji na mmomonyoko wa maadili.

Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania jimbo la kusin magharibi  Mch Robert Pangani(picha na Deus Mellah)
Sauti ya askofu Robert Pangani

Aidha mwakilishi wa  mkuu wa mkoa wa mbeya ambaye ni mkuu wa wilaya ya chunya kamishina msaidizi wa jeshi la uhamiaji Mbaraka Batenga amelishukuru jukwaa hilo la wakristo kwa kuona umhimu wa kuombea mkoa na taifa kwa ujumla.

Mwakilishi wa  mkuu wa mkoa wa mbeya ambaye ni mkuu wa wilaya ya chunya kamishina msaidizi wa jeshi la uhamiaji Mbaraka Batenga
Sauti ya mkuu wa mkoa wa mbeya ambaye ni mkuu wa wilaya ya chunya kamishina msaidizi wa jeshi la uhamiaji Mbaraka Batenga

Akizungumza kwa niaba ya sanjari na hayo  mch Osia Mbotwa mwenyekiti wa kanisa la Moravian wilaya ya Mbeya akimwakilisha mwenyekiti wa jukwa la wakristo mkoa wa Mbeya amesema lengo la maombi hayo ni kuomba kwa Mungu ili kuondoa ajali za mara kwa mara mkoani humo.

Sauti ya mch Osia Mbotwa mwenyekiti wa kanisa la Moravian wilaya ya Mbeya

Nao baadhi ya wachungaji na wakristo walioshiriki katika maombi hayo wameomba maombi hayo yawe endelevu.

Baadhi ya sauti za washiriki wa ibada ya maombi