Baraka FM
Baraka FM
2 April 2026, 10:34

Amani ni tunda la roho kibiblia,hivyo kila mtu anaowajibu wa kulinda na kutunza Amani eneo alilopo.
Na Hobokela Lwinga
Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania mhashamu Conrad Nguvumali Sikombe ameongoza ibada ya maombi ya kuliombea taifa.

Ibada hiyo imefanyika katika kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ushirika wa Nzovwe jumapiili machi 29,2026.
katika ibada hiyo askofu Sikombe amesema taifa limepotoka linahitaji rehema za Mungu iwe kwa viongozi,kanisa na taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine amesema taifa linapokosa amani husababisha shughuli za maendeleo kusimama iwe ndani ya familia hadi maendeleo ya nchi.
Sambamba na hayo amesema viongozi waliopewa nafasi katika uongozi wanapaswa kuwa wakweli na kutenda haki ili kulinusuru kanisa,taifa na machafuko.
Aidha katika mahubiri yake amesistiza waumini kuishi maishi matakatifu yanayompendeza Mungu ikiwa ni pamoja na kutenda mema.
