Baraka FM
Baraka FM
9 March 2026, 23:19

Katika kuadhimisha sikuku ya mama Duniani taasisi ya King James Pharmacy wameamua kutoa msaada wa vifaa vya matibabu katika hospital ya Rufaa kanda ya Mbeya
Na Ezra Mwilwa
King James Pharmacy Yaweka Alama ya Kipekee MZRH, Yaonyesha Kiu ya Wazawa Kuikwamua Sekta ya Afya.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH), leo imepokea msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi Milioni 103 kutoka kwa Uongozi wa King James Pharmacy ya jijini Mbeya katika kuunga mkono juhudi za Serikali katika maboresho ya huduma ya afya nchini.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Mkurugenzi wa King James Pharmacy, Dkt. Gloria Mbwile ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Saia Suluh Hassan Rai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mapinduzi makubwa katika sekta ya afya .
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji ameeleza kufarijika sana na hatua hiyo ya kizalendo.

Nao watumiaji wa vifaa hivyo, Muuguzi Mkuu wa Hospitali, Petro Semen, pamoja na Seraphine Mushi Mkuu wa Kitengo cha fiziotherapia, wamesema kuwa vifaa hivyo vya kisasa vitaongeza ufanisi na kupanua wigo wa utoaji huduma kwa wagonjwa, huku wakiahidi kuvitunza ili vidumu kwa muda mrefu.
Msaada huo uliotolewa maalum katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, unajumuisha vifaa muhimu kwa ajili ya Idara ya Tiba kwa Vitendo (Physiotherapy), Wodi ya Watoto, pamoja na Kitengo cha Uangalizi Maalum (ICU).